
NDAKI YA TIBA ZA MIFUGO NA SAYANSI ZA AFYA IMETAKIWA KUTUMIA VYOMBO VYA HABARI ILI WANANCHI WAWEZE KUFAHAMU SHUGHULI WANAZOFANYA- DR HENRY BWILLE
Na Amina Hezron,Morogoro
Mwenyekiti wa Ndaki ya Tiba za Mifugo na Sayansi za Wanyama VET ameitaka ndaki hiyo kujitangaza kupitia vyombo vya habari ili wananchi waweze kufahamu shughuli zinazofanywa na ndaki hiyo na jamii kuweza kufaidika.
Akizungumza na SUAMEDIA leo Mwenyekiti Dr Henry Bwille amesema kuwa katika ndaki hiyo kuna mambo mengi yanayofanyika ambayo yanaweza kusaidia jamii ambayo mpaka sasa haifahamu kama mambo hayo yanafanyika SUA ndani ya ndaki hiyo.
"Yale maswala yote yanayotendeka hapa chuoni ambayo yanahusu jamii ambayo jamii inaweza kufaidika hata Tanzania nzima kwa ujumla ningeomba wajitangaze ili kuweza kufikia muafaka wa taarifa zetu zijulikane hata wakipata shida waweze kutukimbilia,nimeona kuna dawa za mitishamba zimetengenezwa zinatibu vidonda vya tumbo, vidonda sugu hadi kisukari cha wanyama lakini nnje watu hawajui wanajua wao wenyewe tu", alisema Dr Bwille.
Aidha Mjumbe wa Bodi ya ndaki hiyo ambae muwakilishi wa wajumbe wengine wa bodi Dr Abdu Hayghaimo amemshukulu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA Prof Raphael Chibunda kwakuwawezesha kutembelea sehemu mbalimbali za ndaki hiyo ambazo zinatoa mafunzo kwa wanafunzi ambao wanakwenda katika tiba za udaktari pamoja na tiba zingine lakini pia na kuwanufaisha wakulima wanaozunguka eneo la chuo.
Pia amewaomba kuzingatia yale walioelezwa na mwenyekiti wa bodi hiyo kwakuwa ndaki hiyo inahuduma nzuri na uwezo mkubwa wa kutambua chanzo na sababu za magonjwa kitu ambacho wananchi hawakifahamu hivyo wajitahidi kujitangaza ili wananchi waweze kufaidi huduma zitolewazo hapo.
Kwa upande wake Rasi wa ndaki ya Tiba za Mifugo na Sayansi za Wanyama Prof Amandus Muhairwa amepokea vizuri mawazo yaliyotolewa na mwenyekiti wa bodi na ameahidi kuyafanyia kazi kwa haraka ili mambo yaweze kwenda kama ilivyopendekezwa.
"swala la kujitangaza na kuifanya ndaki yetu ieleweke kwa wadau hiyo ametupatia changamoto kubwa ambayo tunakwenda kuifanyia kazi, ni kweli tunafanya mambo mengi lakini ni wazi kwamba hayajulikani kiasi ambacho inapaswa katika jamii yetu", alisema Prof Muhairwa.

WAZIRI WA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA PROF. JOYCE NDALICHAKO AMEZITAKA TAASISI ZA ELIMU NCHINI KUWA MSTARI WA MBELE KATIKA KUIMARISHA SEKTA YA MICHEZO
Na AYOUB MWIGUNE NA AMINA HEZRON
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amezitaka Taasisi za Elimu nchini kuwa mstari wa mbele katika kuimalisha sekta ya michezo kwenye Taasisi kwani kutaimalisha afya pamoja na kuinua viwango vya elimu na uwajibikaji nchini.
Waziri huyo ameyasema hayo wakati wa kufunga michezo ya Wafanyakazi wa wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA na kuzindua uwanja wa mchezo wa kikapu katika Kampasi Kuu ya Chuo hicho ambapo amesisitiza kuwa michezo ni chanzo cha afya bora kwa watu wote na kuzitaka taasisi kuhakikisha zinatambua umuhimu wa michezo na kuipa kipaumbele
Naye Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA Pro. Raphael Chibunda amesema kukamilika kwa mashindano hayo kumeboresha mahusiano kati ya wafanyakazi wa chuo hicho pamoja na wanafunzi huku pia akishukuru Benki ya CRDB kwa kuendelea kushirikia na na chuo hicho katika nyanja mbalimbali huku akiwaomba kuendelea kushirikiana na chuo cha sokoine ili kuweza umoja na kuwa karibu na wateja wake ambao ni wanajumuiya hiyo
Kwa upande wake Mkurugenzi wa wateja wa Benki ya CRDB Morogoro Prosper Nambaya kama mdau ambaye pia amejitokeza katika kuhakikisha uwanja wa michezo wa mpira wa kikapu unakamilika amesema wao kama benki watahakikisha wanaendelea kutoa sehemu ya faida katika kusaidia jamii na miradi mbalimbali

SHULE ZOTE ZENYE MCHEPUO WA KILIMO NCHINI KUHAKIKISHA ZINAKUWA NA UWEZO WA KUZALISHA MAZAO YA CHAKULA- PROF. NDALICHAKO
Na: Gerald Lwomile
Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imesema itahakikisha shule zote zenye mchepuo wa Kilimo nchini kuhakikisha zinakuwa na uwezo wa kuzalisha mazao ya chakula kwani hiyo ndiyo njia sahihi ya kufahamu kilimo na namna kinavyofanyika.
Akizungumza na wanafunzi na waalimu wa Shule ya Sekondari ya Kilimo iliyoko Kilosa Mkoani Morogoro Novemba Mosi, 2019 Waziri Profesa Ndalichako amesema Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt John Pombe Magufuli inataka kuhakikisha hakuna uhaba wa chakula katika shule hizo.
Amesema awali katika shule nyingi zenye mchepuo wa kilimo hazikuwa hata na mashamba na kushangaa inawezekana vipi shule wanafunzi wanasoma mambo ya kilimo lakini hakuna hata shamba linaloonyesha kuwa kweli kuna masomo ya kilimo.
Katika hatua nyingine Waziri huyo wa Elimu,Sayansi na Teknolojia, amewaonya Maafisa Elimu wa Mikoa yote hapa nchini wanaomdanganya Rais kuwa wamemaliza tatizo la upungufu wa madarasa na badala yake wanaongeza idadi ya wanafunzi katika shule na kusababisha wanafunzi hao kufanya vibaya katika matokeo ya mtihani wa mwisho.
Amesema vitendo hivyo vinasababisha walimu wa shule hizo kushindwa kufundisha kwa ufanisi na matokeo yake wanafunzi kushindwa kufanya vizuri katika masomo yao.
Akizungumzia ukarabati unaofanywa na Wizara yake katika Shule ya Sekondari ya Kilimo ya Kilosa ambayo imepewa zaidi ya shilingi milioni 750 amesema ukarabati huo ni kuigwa kwani sasa shule inamuonekana mzuri huku kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 150 kikiwa kimebaki
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Adam Mgoya amesema kuwa mafanikio ya ukarabati huo unatokana na ofisi yake kusimamia kwa karibu zaidi ili kuhakikisha fedha hizo zilizotolewa na Serikali zinatumika vizuri na kuleta tija katika elimu.

VIDEO:Multisectoral research on sleeping sickness in Tanzania in the context of climate change
Professor Paul Gwakisa of Sokoine University of Agriculture in Tanzania engaged a “OneHealth” approach to research on sleeping sickness, bringing together the health, environment and agriculture sectors. Professor Gwakisa has conducted his research with the support of TDR, the Special Programme for Research and Training in Tropical Diseases, hosted at the World Health Organization.
More information: https://www.who.int/tdr/research/vect...

WATAFITI NCHINI WAMESHAURIWA KUWASILISHA ANDIKO LOLOTE LA UTAFITI KWANZA KWA WADAU WA UTAFITI KABLA YA KUOMBA KIBALI
Amesema kukutana kwao kwenye warsha hiyo lutasaidia sana wakuu wa taasisi kuweza kuwasaidia watafiti wake kuweza kutimiza vigenzo na masharti yaliyowekwa kwa mujibu wa sharia na kanuni za tafiti ili kuwa na Utafiti

SUA YATAKIWA KUENDELEZA VIWANGO VYA ELIMU BORA
Na, Catherine Mangula Ogessa.
Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dar es salaam Mhe. Jaji Mstaafu Damian Lubuva amekitaka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kuendeleza viwango vya ubora wa elimu ambayo imekuwa ikitolewa na chuo hicho, lakini pia akikipongeza chuo hicho kwa kuwa na muonekano wa nje unaoakisi kuwa chuo hicho ni chuo cha Kilimo.
Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dar es salaam Jaji Mstaafu Damian Lubuva akizungumza na Menejimenti ya SUA.
Jaji Mstaafu Lubuva ameyasema hayo wakati wa ziara yake katika Chuo Kikuu SUA, ziara ambayo imekuwa na lengo la kujifunza sanjari na kuimarisha urafiki uliopo baina ya vyuo hivyo viwili, huku akisisitiza vyuo hivyo kila kimoja kutaka kujifunza toka kwa mwenzake kwa lengo la kuboresha utoaji wa huduma.
Amevitaka vyuo hivyo kuendeleza ushirikiano ikizingatiwa kuwa mbali na vyuo hivyo kuwa ni vya umma lakini pia historia iko wazi kuwa chuo cha SUA kimezaliwa toka Chuo cha Dar es salaam, hivyo mahusiano mazuri ya vyuo hivyo sio tu kwa manufaa yao bali ni kwaajili ya Taifa kwa ujumla.
Kwa upande wake Makamu wa Mkuu wa Chuo kikuu cha Dar es salaam Prof. William Andley Lazaro Anangisye amewataka watumishi wa vyuo kuhakikisha wanaweka mbele kwanza maslahi ya vyuo na Taifa kwa ujumla hivyo wasitangulize pesa mbele kwani kwa nafasi zao wanadhamana ya kuleta mabadiliko chanya.
Amefafanu kuwa ni muhimu kila mmoja kuhakikisha anatimiza wajibu wake katika kuhakikisha malengo ya chuo husika yanafikiwa na baadae kunakuwa na kitu kwaajili ya Watanzania ambacho kimefanyika. Lakini pia amebainisha kuwa Chuo Kikuu cha Dar es salaam kimekuwa kinajifunza mambo mengi kutoka SUA.
Aidha katika ziara ya Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dar es salaam pia ameweza kutembelea shamba la mfano, Apopo, Hospitali ya Rufaa ya Wanyama, Maabara ya Sayansi ya udongo, SUA AIC, Hospitali ya Mazimbu pamoaja na Makaburi ya Mazimbu.
Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Prof. William Andley Lazaro Anangisye.

Zaidi ya shilingi bilioni 11 zimetolewa kama mikopo kwa wadau mbalimbali kwenye Sekta ya uvuvi
wa fedha wa 2018/2019 katika benki ya TADB ili kusaidia kuboresha miundombinu na mitaji baada ya kuanzishwa
kwa dawati la sekta binafsi katika wizara hiyo.
Tamatama wakati akizungumza na watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA waliokuwa wanafanya
Utafiti kupitia Mradi wa Ubunifu wa teknolojia mbalimbali na Masoko ya Uvuvi kwa Ziwa Victoria (IMLAF).
TADB kama mikopo kwenda kwenye sekta ya uvuvi lakini bada ya kuanzishwa kwa dawati hilo kumesaidia
kupatikana kwa fedha hizo kwa wadau wa uvuvi na sasa kuna fedha zingine zaidi ya shilingi bilioni 22 zipo kwenye
hatua mbalimbali ili ziweze kukopeshwa kwa wadau.
mbalimbali ya wizara yangu ili kuinua Sekta ya Uvuvi na hivyo nitoe pongezi zangu na za wizara kwa SUA kwa kazi
hii nzuri iliyofanywa na watafiti hao kupitia mradi huo wa IMLAF“ Alisema Dkt. Tamatama.
kuhamasisha wavuvi kujiunga kwenye vikundi ili iwe rahisi wao kokopesheka na tayari wamefanikiwa
kuishawishi benki ya Posta kuanzisha akaunti maalumu inayoitwa Mvuvi akaunti kwaajuili ya vikundi vya wavuvi nchini.
miundombinu bora nay a kisasa ya kukaushia dagaa haoa na hivyo kusaidia kuongeza thamani ya dagaa kwa
kutokuanika kwenye mchanga ambapo soko la Zambia wananunuliwa kilo moja kwa dolla 6 kwa sasa.
cha Kilimo SUA Prof.Raphael Chibunda amesema uvuvi wa dagaaa ni wa siku nyingi katika Ziwa Victoria na hawa
Samaki sio kama wanatumiwa na binadamu pekee lakini pia wanatumika kwenye kutengeneza chakula cha mifugo.
kwa Ziwa Victoria (IMLAF) ulilenga kuboresha mazao ya samaki kutoka kwenye ziwa hilo ili wavuvi wanufaike
zaidia kwenye kazia mbayo wamekuwa awakiifanya.
vichanja na neti umeenea na wavuvi wengi wanatumia na zao la dagaa limeboreka kwahiyo ni matumaini yetu
kuwa mradi unapokaribia mwisho, viongozi wa serikali na wale wa kijamii ambao mradi huu umefika kwenye
maeneo yao wataendelea kuwahimiza wavuvi kutumia njia hizi ambazo ni bora zitakazowaongezea kipato na
kipato cha nchi yetu” Alisisitiza Prof. Chibunda.
wanaopendwa na kutumika Zaidi nchini Tanzania hasa Dagaa ambao soko lake limepanuka na kufika kwenye
nchi mbalimbali za jirani Kongo, Burundi na Zambia na kusaidia nchi kupata fedha za kigeni na kupunguza
Umasikini katika kaya za Wavuvi.

The List Of Batch I Loan Allocation For SUA First Year (Fresher) Students 2019-2020

SUA yabaini Samaki katika Ziwa Victoria na walaji wapo salama kufuatia hofu ya matumizi ya sumu wakati wa uvuvi na utunzaji wa Samaki.

SUA kimeingia mkataba wa makubaliano ya ushirikiano (MoU) na Chuo Kikuu cha Greenwich cha Uingereza kupitia programu ya Mpango wa Usalama wa Chakula na Lishe
Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, SUA kimeingia mkataba wa makubaliano ya
ushirikiano (MoU) na Chuo Kikuu cha Greenwich cha Uingereza kupitia programu
ya Mpango wa Usalama wa Chakula na Lishe (FaNSI) ya Taasisi ya Maliasili (NRI).
Kilimo tarehe 16 Oktoba 2019 yalitanguliwa na uwasilishwaji wa taarifa na historia
fupi za vyuo hivyo viwili.
Lengo la makubaliano hayo ni kushirikiana katika Nyanja mbalimbali ikiwemo
katika Shahada za Uzamivu na kubadilishana uzoefu wa namna ya kuandika
maandiko ya mapendekezo huku Kituo cha Kudhibiti wa Viumbe hai waharibifu
kutoka SUA kikiwa moja ya wadau pekee wa program hiyo katika Nchi za kusini
wa Jangwa la Sahara.
Kupitia makubaliano hayo Mwanataaluma mmoja wa SUA amefanikiwa kupata
ufadhili wa shahada ya uzamivu kwenda kusoma na kujifunza katika Chuo Kikuu
cha Greenwich Januari 2020.
Mkurugenzi wa Kituo cha Kudhibiti wa Viumbe hai waharibifu, Dkt. Ladislaus
Mnyone amekipongeza Chuo kikuu hicho cha Greenwich kwa kufanikisha swala
hilo ambalo litaleta tija baina ya vyuo vyote viwili.
Dkt. Mnyone amewashauri wanafunzi kuchangamkia fursa hiyo hasa kwenye
upande wa tafiti ambazo zinazoweza kutatua changamoto mbalimbali Tanzania na
duniani kwa ujumla.
NRI ni taasisi iliyobobea kwenye tafiti za maendeleo ya kijamii kama Chakula,
Kilimo, Mazingira na Maisha Endelevu ambayo inasimamia programu ya Mpango
wa Usalama wa Chakula na Lishe (FaNSI) ili kutatua changamoto zinazolikumba
bara la Afrika hasa kwenye upatikanaji wa mlo kamili.
Chuo Kikuu cha Greenwich kupitia FaNSI kinafanya kazi na taasisi mbalimbali
barani Afrika ambapo Chuo Kikuu cha Sokine cha Kilimo, SUA ikiwa ni moja ya
taasisi hizo kwa sasa.

Watumishi Mvomero waaswa kuwa waadilifu, kuchapa kazi – DC apewa “rungu”
Na Andrew Chimesela - Morogoro
Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero na wale wanaofanya kazi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo wameaswa kufanya kazi kwa bidii, uaminifu na uadilifu kwa kuwa hiyo ndiyo silaha pekee kwa Mtumishi wa Umma.
Nasaha hizo zimetolewa Oktoba 15 mwaka huu na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Loata Ole Sanare alipokuwa anazungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo ikiwa ni mwendelezo wake wa kujitambulisha kwa kila Halmashauri na kuzungumza na watumishi ili kusikiliza changamoto walizonazo na kuzitafutia ufumbuzi.
Amewataka watumishi hao kusimama imara katika kufanya kazi na kutumia weledi wao kwa kwa ajili ya kuwatumikia wananchi na kwamba uadilifu ndiyo silaha muhim katika kufanya kazi ya Umma.
“Uadilifu katika kufanya kazi ni kitu kizuri sana, msishangilie kwa sababu mmeona wengine na kweli walimopita mmeona kilichotokea, sasa aje hapa akute tuko wamoja na tunachapa kazi” alisema Mhe. Sanare.
Hata hivyo Mhe. Sanare anaendelea kuwakumbusha watumishi wote wa Umma kutumia vema rasilimali za Serikalizilizopo iwe fedha za kutoka Serikali Kuu ama fedha zinazokusanywa na Halmashauri.
Amesema mtumishi atakayetumia vibaya rasilimali hizo atahesabika adui namba moja wa Serikali na Halmashauri anayofanyia kazi huku akibainisha kuwa mtumishi wa aina hiyo kamwe hatohamishwa badala yake ataachishwa kazi, hilo likiwa pia ni agizo kwa Mkuu wa Wilaya hiyo MHe. Mwalimu Mohamed Utali kuwaweka kando wabadhirifu wote wa mali ya Serikali ndani ya Wilaya yake.
Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo amewataka watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero kufanya kazi kwa Ufasaha, kwa Ufanisi na kwa wakati na kwamba hayo yatawezekana tu pale mtumishi atakapoamua kufanya kazi kwa uwazi.
Akiwajengea kujiamini zaidi Mhandisi Kalobelo amewataka watumishi hao kujijengea tabia hiyo ya uwazi itamsaidia kushirikisha wengine pale anapokutana na changamoto katika utekelezaji wa majukumu yake.
Amesema ni jambo jema kwa Mtumishi wa Serikali kumshirikisha kiongozi wake mapema au mtumishi mwenzake yeyote ili kusaidiwa changamo anayokumbana nayo badala ya kubaki nayo kwa muda mrefu na ri utendaji wake wa kazi na wa taasisi yake.
Tayari Mkuu wa Mkoa Mhe Loata Sanare akiambatana na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ngazi ya Mkoa amekwisha tembala Halmashauri tatu kati ya Halmashauri tisa za Mkoa huo.
Subcategories
Page 1 of 52